VIRUSI VYA HOMA YA INI [HEPATITIS]

Billyblogtz
0

          VIRUSI VYA HOMA YA INI [HEPATITIS]


Virusi vya homa ya Ini
Ugonjwa wa homa ya ini ni hatari kuliko ukimwi,uwezekano wa mtu kupata maambukizi ya virusi vya homa ya ini ikiwa atajamiana na mtu mwenye virusi hivyo ni mara 10 zaidi ikilinganishwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Takwimu zinaonesha zilizotolewa mwanzoni mwa mwaka huu nchini ni kuwa watu nane kati ya 100 nchini wana maambukizi ya virusi vya homa ya ini hususani hepatitis B.

Saratani ya ini inasababishwa na nini?.
Ugonjwa huu unaweza kusababishwa na vitu  vifuatavyo
1.saratani ya ini inayotokana na kuzidi sumu kwenye ini [toxic hepatitis]
Hii inaweza sababishwa na madawa ,utumiaji pombe kupita kiasi,sumu za viwandani,sumu za miti.

2.saratani inayotokana na unywaji wa pombe kupita kiasi [alcholic hepatitis]
Hii inaweza kuwa sugu au isiwe sugu na inaweza kutibika ikiwa mtu ataacha matumizi yapombe yaiofaa.na hii ndio inaweza kusababisha kulika/vidonda kwenye ini.


3.saratani inayosababishwa na virusi [viral hepatitis]
Hapa tuna tizama virusi wanaosababisha ugonjwa huu ambao ni
Virusi vya hooma ya ini aina A [HEPATITIS A],virusi vya homa ya ini aina B [HEPATITIS B],Virusi vya homa ya aini aina C [HEPATITIS C],virusi vya homa ya ini aina  D [HEPATITIS D] NA HEPATITIS E




JINSI  UNAVYOAMBUKIZWA:
Katika maeneo hatari zaidi duniani, Virusi vya Hepatitis B (HBV) kwa kawaida husambazwa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kuzaliwa au kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine hususan nyakati za utotoni.

Kama ilivyo kwa Ukimwi, Virusi vya Homa ya Ini pia huambukizwa kwa njia ya kujamiiana, mate, jasho na mwingiliano wowote ule wa damu.

Njia  kuu  za  maambukizi :
-Kujamiana bila kinga
-Kunyonyana ndimi 'denda'
-Mama mwenye ugonjwa kumwambukiza mtoto wakati wa  kujifungua
-Kuchangia damu isiyo salama
-Kuchangia vitu vya ncha kali kama sindano, wembe n.k
-Kuchangia miswaki
-kuchangia taulo na mwenye ugonjwa huo
-kubadilishana nguo au kukumbatiana wakati mkiwa mnavuja jasho.

Mtu mwenye Homa ya Ini ana wastani mdogo wa kuishi kuliko mwenye Ukimwi. Kwa maana hiyo, mwenye maambukizi ya Virusi vya Homa ya Ini hufariki dunia haraka kuliko mwenye VVU.


Dalili za saratani ya ini.

•Liver  Cirrhosis (vidonda kwenye ini).
·         Watu wengi hawaonyeshi dalili yoyote. Kwa maana hiyo mtu anaweza kuishi na HBV na kusababisha maambukizi kwa wengine bila kugundulika.

·         Hata hivyo, watu wengine husumbuliwa na homa kali na dalili ambazo hudumu kwa wiki kadhaa. Dalili hizo ni:
 -Uchovu
-Kichefuchefu
-Mwili kuwa dhaifu
-Homa kali
-Kupoteza hamu ya kula
-Kupungua uzito
-Maumivu makali ya tumbo upande wa ini
-Macho na ngozi kuwa vya njano
-Mkojo mweusi

Kwa wagonjwa wengine, Virusi vya Hepatitis B hukua hadi kusababisha ini kuharibika kabisa (cirrhosis of the liver) au saratani ya ini (liver cancer).


matibabu ya virusi vya homa ya ini
Gharama za kutibu ugonjwa huu ni kubwa  na ni vyema jamii ikajikinga na ugonjwa huu hatarishi.
Alisema ummy mwalimu “kinga ni bora kuliko tiba ,tiba kwa wagonjwa waliopata kirusi aina A NA E ,mara nyingi hutolewa kutokana na dalili zinazoambatana na ugonjwa huu” kwa wagonjwa waliogundulika kuwa na hepatitis B na C matibabu hutegemea na hatua aliofikia.


Kinga ya ugonjwa huu
1.Chanjo/kinga .Kinga hii hutolewa kwa mtu ambae hana maambukizi ya virusi hawa.
Na chanjo iliopo kwa Tanzania ni ya hepatitis  B.Chanjo ya hepatitis A inapatikana baadhi ya nchi
Na hakuna chanjo kwa hepatitis C,D na E.
2.Kuepuka matumizi ya madawa ya kulevya
3.kuepuka uasherati
4.kujiepusha matumizi mabaya pombe
-Kuacha kuchangia vitu vya ncha kali kama sindano, wembe n.k
-Kutochangia miswaki






KUNDI LIPI NI HATARI ZAIDI?
Asilimia 80-90 ya watoto wachanga ambao huambukizwa katika kipindi cha mwaka wa kwanza tangu kuzaliwa, Homa ya Ini hukua mpaka kufikia kuwa sugu na hatimaye kifo.

Asilimia 30-50 ambao huambukizwa kabla ya kufikisha umri wa miaka sita, Hepatitis B hukua mpaka kuwa sugu na baadaye ni kifo.
 
Asilimia 90 ya watu wazima wanaopata HBV, virusi hivyo hutoweka ndani ya miezi sita. Yaani uimara wa ini husababisha virusi hivyo kupotea.

Asilimia tano kushuka chini ya watu wazima wanaopata maambukizi ya HBV, virusi hivyo vya Hepatitis B kugeuka sugu na hatimaye kifo.
 
Asilimia 15-25 ya watu wazima ambao walipata maambukizi utotoni na hatimaye Hepatitis B kuwa sugu, hufariki dunia kutokana na matokeo ya ini kuharibika kabisa au kwa saratani ya ini.
 
TANZANIA IPO KUNDI  HATARISHI
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), Kusini ya Jangwa la Sahara ndiyo eneo hatari zaidi. Tanzania ni moja ya nchi zilizopo katika eneo hilo. Kiwango cha hatari Kusini ya Jangwa la Sahara kinalingana na kile cha Mashariki ya Bara la Asia.
 
Ripoti hiyo inaonesha kuwa watu wengi walipata maambukizi nyakati za utotoni na kwamba kati ya asilimia tano mpaka 10 ni waathirika sugu.

         na ini zima kabla ya kupata mardhi haya latakiwa kuwa nmna hii

read more other disease
Tags

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)

#buttons=(Ok, Go it!) #days=(1)

Our website uses cookies to enhance your experience. Check Now
Ok, Go it!